Joshua 16:1-4

Mgawo Kwa Efraimu Na Manase

1 aMgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli. 2 bUkaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi, 3 cukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 dKwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.

Copyright information for SwhNEN